Wednesday, 8 May 2013

BALOTELLI ANG'ARA NA KUIWEZESHA AC MILAN KUFUZU KUCHEZA UEFA BAADA YA KUIFUNGIA BAO 2 KATIKA USHINDI WA 4-0 DHIDI YA PESCARA

MTALIANO Mario Balotelli amefunga mabao mawili usiku huu ikiwemo penalti babu kubwa, akiiwezesha AC Milan kupata nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuichapa Pescara mabao 4-0.
 
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester City alifunga bao lake la kwanza kwa penalti kabla ya kufunga lingine katika mechi ambayo wachezaji wengine waliowahi kucheza Ligi Kuu ya England Sulley Muntari na Mathieu Flamini walifunga.
 
Amekuwa na mafanikio tangu arejee Italia na Milan wamekuwa hawafungwi katika mechi ambazo anacheza Serie A, ikishinda nane na kutoa sare tatu. 
 
Deadly: Mario Balotelli slots home the first of his brace from the penalty spot
Mario Balotelli akifunga kwa mkwaju wa penalti
 
Top draw: Balotelli and Robinho celebrate going ahead against bottom side Pescara
Balotelli akishangilia na Robinho
 
Premier League connection: Sulley Muntari also got his name on the scoresheet
Waliocheza England wanatisha: Sulley Muntari akishangilia bao lake
 
Up for a fight; Balotelli tussle's with Pescara's Marco Capuano in his usual combative style
Balotelli akimtoka Marco Capuano 
 
Bowing to the crowd: Milan players decide to show their appreciation to the supporters
Wachezaji wa Milan wakishangilia