Chama   Cha Mapinduzi(CCM) mkoani Arusha kimelitaka jeshi la polisi mkoani  hapa  sanjari na vyombo mbalimbali vya usalama kufanya uchunguzi wa kina  na  haraka ili kubaini chanzo cha kifo cha mwanafunzi wa chuo cha  uhasibu  Arusha (IAA),Henry Kago(22)  aliyefariki hivi karibuni baada ya    kuchomwa kisu na watu wasiojulikana.
Pia,chama  hicho kimeitaka  serikali kusimamia na kumaliza haraka uchunguzi ambao  utawezesha  shughuli za kimasomo kuendelea katika chuo hicho  na kutaka  wale wote  waliohusika na vurugu hizo wachukuliwe hatua kali za  kisheria.
Akizungumza  na waandishi wa  habari katibu mwenezi wa chama hicho mkoani  Arusha,Isaack Joseph maarufu  kama Kadogoo alisema kuwa chama chao   kinalaani vikali tukio la vurugu  zilizojitokeza katika chuo hicho na  kimepokea kwa masikitiko makubwa  kifo cha mwanafunzi huyo.
Alisema  kuwa tukio la kuuwawa  kwa mwanafunzi huyo ni tukio la kinyama na  waliotekeleza hawakujali uhai  wa kijana huyo ambaye alikuwa ni nguvu  kazi ya taifa  na kuitaka  serikali kuwabaini waliohusika mara moja.
“Chama  kimefikia hatua hiyo  kutokana na tukio hilo la kinyama linalodaiwa  kufanywa na watu wasiojali  uhai wa watu wengine hususani kijana ambaye  ni nguvu kazi ya  taifa”alisema Joseph
Alisema  kuwa wao kama chama  wanaitaka serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi  na usalama kuchunguza  kwa kina taarifa za tukio hilo ili kubaini  ukweli na kuwachukulia hatua  wahusika wote waliopanga mauaji ya  mwanafunzi huyo.
Hatahivyo,alisisitiza  kwa  kuitaka serikali kusimamia na kumaliza haraka uchunguzi ambao  utawezesha  shughuli za kimasomo kuendelea chuoni hapo na kuwataka  wanafunzi wa  vyuo mbalimbali nchini kutambua kile kilichowapeleka  chuoni hapo.
“Chama  kinawaonya  wanafunzi  wote katika vyuo mbalimbali nchini kutambua  kilichowapeleka katika vyuo  hivyo na kuachana na ushawishi wa wanasiasa  wanaowaondoa katika malengo  yao ya msingi ya kujipatia  elimu”alisisitiza Joseph
Hatahivyo,alilipongeza  jeshi  la polisi mkoani Arusha kwa kazi nzuri ya kulinda raia na mali  zake   hususani katika tukio la vurugu lililojitokeza chuoni hapo huku  akidai  wao watendelea kutoa ushirikiano kwa ufanisi na uweledi mkubwa.
JAMII BLOG 

 
 



 
 
 
 
 
 
